Majeshi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), yameanza kutoa huduma mbalimbali za kijamii na kibinadamu kwa wananchi wa Tanzania ikiwemo matibabu ya bure kutoka kwa madaktari bingwa wa nchi za Burundi, Somalia, Tanzania, Rwanda, Kenya, na Uganda.
Jumatano, Agosti 26, 2026

Dar es Salaam. Majeshi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), yameanza kutoa huduma mbalimbali za kijamii na kibinadamu kwa wananchi wa Tanzania ikiwemo matibabu ya bure kutoka kwa madaktari bingwa wa nchi za Burundi, Somalia, Tanzania, Rwanda, Kenya, na Uganda.
Hatua hiyo ni sehemu ya Maadhimisho ya Sita ya Wiki ya Ushirikiano wa Majeshi ya Nchi Wanachama wa Jumuiya hiyo yaliyoanza leo Agosti 26, hadi Septemba Mosi, 2026 hapa nchini.
Aidha, maadhimisho hayo yanahusisha shughuli za ukarabati na utoaji wa misaada ya kijamii katika vituo vya afya, vituo vya kulelea watoto yatima, na Magereza katika Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Arusha, na Zanzibar.
Baadhi ya vituo vitakavyonufaika na huduma na ukarabati huo ni pamoja na Hospitali ya Wilaya ya Ubungo, Hospitali ya Vijibweni Kigamboni, na Kituo cha Afya Yombo Malawi (Dar es Salaam), Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi na Hospitali ya Wilaya Bagamoyo (Pwani), pamoja na Hospitali za Wilaya za Mwerapongwe Unguja na Vitongoji Pemba.
Akizungumza katika uzinduzi huo leo Jumatano, Agosti 26, 2026, Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Salum Haji Othman amesema ushiriki wa majeshi kutoka nchi mbalimbali za Afrika Mashariki ni ishara ya umoja wa kikanda na dhamira ya majeshi hayo ya kuhudumia wananchi.

"Tanzania inafurahia kuwa mwenyeji wa vikosi kutoka Burundi, Kenya, Uganda, Somalia na nchi nyingine washirika ushirikiano huu unaimarisha uhusiano kati ya majeshi na wananchi pamoja na kubadilishana uzoefu katika operesheni mbalimbali," ameeleza.
Mnadhimu huyo Mkuu wa JWTZ amesema ushirikiano unawawezesha wanajeshi kutoka nchi mbalimbali kubadilishana uzoefu, kuimarisha utayari na kuongeza uwezo wa kufanya kazi kwa pamoja.
“Licha ya mipaka yetu ya kitaifa, sisi ni eneo moja lililoungana katika kuwatumikia wananchi,” amesema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Utawala wa JWTZ, Brigedia Jenerali Dk Agatha Katua amebainisha kwamba zoezi hilo siyo la kwanza kwani kwa upande wa Tanzania ni mara ya pili kwa kuwa mara ya kwanza lilifanyika mwaka 2022.

"Kwa mwaka huu Septemba Mosi ndio siku tunayo timiza miaka 62 ya jeshi la JWTZ. Kwa hiyo wiki moja kabla tunafanya moja ya njia za kuadhimisha ni pamoja na kuwa na zoezi hili ambalo linashirikisha majeshi ya nchi za Afrika Mashariki kutoa huduma kwa jamii ili kujenga mahusiano mazuri na jamii zinazotuzunguka" ameelezea.

Kupitia zoezi hilo, misaada itawafikia wafungwa katika Gereza la Segerea jijini Dar es Salaam na Gereza la Kisongo Mkoani Arusha, sambamba na vituo vya kulelea watoto yatima vya Kurasini, Mwandaiwa Orphanage Centre Bunju, Chanika Children Shelter (Dar es Salaam), SOS Orphanage Centre Zanzibar, na vituo vya afya vya Kibokoni Pemba na Mapinduzi Dodoma, Chamwino.
| # | Наименование новости | Тональность | Информативность | Дата публикации |
|---|---|---|---|---|
| 1 | China kuisaidia Tanzania usimamizi mashirika ya umma | 0 | 4.56 | 26-08-2026 |
| 2 | Tanzania Chairs Regional Labour Migration Committee | 0 | 6.08 | 18-08-2026 |
| 3 | MBEGU YA UCHUMI: Kugeuza umeme wa ziada kuwa fursa ya kiuchumi | 0 | 7.3 | 27-08-2026 |
| 4 | Koffi Olomide ana historia ndefu Tanzania | 0 | 8.26 | 28-08-2026 |
| 5 | РФ обсуждает с некоторыми странами заключение договоров о выдаче преступников | 0 | 0 | 06-05-2025 |
| 6 | Несырьевой неэнергетический экспорт Москвы в Африку за восемь месяцев вырос в 1,5 раза | 0 | 0 | 17-11-2021 |
| 7 | Magoti azindua kampeni chanjo ya polio Kisarawe | 0 | 7.3 | 27-08-2026 |
| 8 | UCHAMBUZI WA MJEMA: Tusijidanganye, tunahitaji maandalizi haya kabla ya 2030 | 0 | 18.33 | 27-08-2026 |
| 9 | Культурно-деловые миссии Петербурга пройдут в 2024 году в четырех странах Африки | 0 | 0 | 31-07-2023 |
| 10 | Страны БРИКС надеются на устойчивое урегулирование конфликта на Украине | 0 | 0 | 29-04-2025 |